Top Ad unit 728 × 90

PICHA MBALIMBALI ZA UOKOAJI WA MIILI YA WATU BAHARINI


Waokoaji wakiwa kazini kwenye Meli ya Kilimanjaro



Muokoaji akiwa na maiti


Waokoaji wakiwa na majeruhi kwenye moja ya Boti za uokoaji.


Majeruhi wa wakipatiwa matibabu kwenye Hospitali ya Mnazi Mmoja


MV KMKM ikiwa kazini


Raia wa kigeni wakiwasili Bandarini baada ya kuokolewa


Majeruhi wakipatiwa matibabu katika Hospitali ya Mnazi Mmoja







Mamlaka ya Udhibiti Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (SUMATRA) imesema, meli iliyozama jana katika kisiwa cha Chumbe, Zanzibar ilikuwa na abiria 248 wakiwemo watoto 31. 

Kwa mujibu wa Sumatra, meli hiyo, inamilikiwa na Kampuni Seagul Transport, imasajiliwa na Mamlaka ya Usafiri Baharini Zanzibar (ZMA) na kwamba, Cheti cha Ubora kimeanza tarehe 24 Agosti, 2011 na kinamalizika 23 Agosti, 2012. Imesema, meli hiyo ilikuwa imeruhusiwa kubeba abiria wanaoruhusiwa 300 na tani 26 za mizigo.

SUMATRA kupitia Kituo cha Utafutaji na Uokoaji (MRCC) ilipata taarifa kuwa meli ya MV Skagit iliyokuwa safarini kutoka Dar es Salaam kuelekea Zanzibar ilikuwa inazama katika eneo la karibu na kisiwa cha Chumbe, Zanzibar, eneo ambalo lipo umbali wa Kilomita za Bahari 13.8 kutoka Bandari ya Zanzibar.

Zoezi la uokoaji linaendelea katika eneo la tukio kutoka kwa Mv Flying Horse, Mv Kilimanjaro III, Tug Bandari ya Zanzibar, KMKM, Mv Zanzibar I, Police Patrol Boat, Navy.


Chanzo:www.francisgodwin.blogspot.com
PICHA MBALIMBALI ZA UOKOAJI WA MIILI YA WATU BAHARINI Reviewed by Unknown on Thursday, July 19, 2012 Rating: 5

No comments:

All Rights Reserved by Dj Mchomo © 2014 - 2015
Powered By WordPress24x7

Contact Form

Name

Email *

Message *

Dj Mchomo. Powered by Blogger.