Top Ad unit 728 × 90

SAJENT AMSHUKIA NAY WA MITEGO

STAA wa filamu Bongo, Husna Idd ‘Sajent’ amemvaa mkali wa Bongo Fleva, Emmanuel Elibariki  ‘Nay wa Mitego’ na kusema wimbo wake uliolenga kuwachafua Bongo Movies, ulipaswa uwe wa wanamuziki na si wao.
Akizungumza na Tollywood Newz, Sajent alisema amesikitishwa na wimbo wa Nay uitwao Nasema Nao ambao ndani yake kuna mashairi ya kuwaponda wasanii wa filamu kuwa ndiyo wanaoongoza kwa umalaya.
“Hata siku moja nyani hajawahi kuona makalio yake, yeye ataendelea kuwacheka wenzake kuwa wana makalio mekundu, lakini hajayaona yake.
“Ni sawa na Nay sasa. Yeye ni mropokaji, anatafuta njia ya kujipaisha kisanii. Sasa jamani, hivi sisi wa filamu na wao (Bongo Fleva)  ni akina nani wanaongoza kwa umalaya? Atasema sana, lakini ukweli utabaki palepale na huyo Nay mwenyewe anauja ukweli.”

SAJENT AMSHUKIA NAY WA MITEGO Reviewed by Unknown on Wednesday, September 26, 2012 Rating: 5

No comments:

All Rights Reserved by Dj Mchomo © 2014 - 2015
Powered By WordPress24x7

Contact Form

Name

Email *

Message *

Dj Mchomo. Powered by Blogger.