Top Ad unit 728 × 90

Msikilize Noorah na Ukimya wake katika Muziki

Msanii Noorah ameongelea mengi kuhusiana na kwa nini yupo kimya sana katika game la muziki wa bongo..Noorah ameyasema yake mengi wakati akihojiwa katika Kipindi cha Fleva GX ya Impact FM ambapo alielezea hasa ukimya wake unatokana na nini.

Kikubwa zaidi Noorah alisema kwamba toka kitambo alikuwa anafanya muziki lakini ndoto zake hazikuwa katika muziki kama tulivokuwa tukidhania lakini aleweza kueleza kwamba ana ndoto zake tofauti na Muziki ambazo zinamfanya akae kimya sana japo siku za hivi karibuni alitoa track aliyomshirikisha msanii Alikiba.

Pia msanii Noorah aliweka wazi kuhusiana na suala la Record Lebel kwa wasanii na studio za kibongo kwa kusema kuwa kwa Bongo bado hakuna Studio ambao wanatimiza ile maana ya kuwa Lebel na wasanii fulani kwa kudai kuwa hakina studio hata moja ambayo inakuwa tayari kumhudumia msanii wake vitu mbalimbali akitolea mfano wa MATIBABU hasa pale msanii husika anapoumwa. Kutokana na studio nyingi kuwa hazifanyi vitu kama hivo kwa hapa Tanzania basi Noorah akasema bado hatuna Record Lebel hapa Bongo zaidi ya kwamba wote ni wazugaji tu kwani hawatimizi yale yanayotakiwa kufanywa. Alieleza hayo yote wakati alipoulizwa swali kwamba yeye yupo Lebel gani kwa hapa Bongo...ndipo alipofunguka hayo..

Msikilize hapa down na yale mengi yaliyokupita wewe ambaye ulikosa show.

Msikilize Noorah na Ukimya wake katika Muziki Reviewed by Unknown on Thursday, March 14, 2013 Rating: 5

No comments:

All Rights Reserved by Dj Mchomo © 2014 - 2015
Powered By WordPress24x7

Contact Form

Name

Email *

Message *

Dj Mchomo. Powered by Blogger.