YOUNG KACHA KUACHIA NGOMA NA DARASA MWISHONI MWA MWEZI HUU!
Msanii Young Kacha toka studio za Street Sound anajiandaa kutoa track yake mpya itakayotoka mwishoni mwa mwezi huu ambayo amefanya collabo na Mr Sikati Tamaa a.k.a Darassa ambaye amesimama vizuri katika Verse ya Tatu ya ngoma hiyo.
Msanii mwingine aliyeshirikiswa katika song hilo ni Milthana ambapo Young Kacha mwenyewe Karap katika verse mbili za mwanzo na Milthana chorus kisha Darasa kumaliza na verse ya tatu na mwisho.
Mzigo umesimamiwa pale pale Street Sound chini ya Producer aliyegonga ngoma ya mwanzo pia ya Young Kacha ya Go 2 Hell mtu mzima B Bash kisha final mixing na mastering amekaa mwenyewe Young Kacha ambaye nae kwa sasa ni kati ya Maproducer wanaokuja kwa kazi na mkono wake wa kwanza ulikuwa katika ngoma ya TASH 'Una Gundu'.
YOUNG KACHA KUACHIA NGOMA NA DARASA MWISHONI MWA MWEZI HUU!
Reviewed by Unknown
on
Friday, April 12, 2013
Rating:
No comments: