Top Ad unit 728 × 90

KALA PINA NA NASH MC WAELEZA NINI CHANZO CHA KUPIGWA KWA CHID BENZ

Baada ya muasisi wa harakati za hip hop Tanzania Kalapina kumchapa Rapper Chidi Benz katika jukwaa la maisha club hapo jana, Kalapina ameelezea sababu za kutoa dozi hiyo kwa msanii mwenzake, hichi ndicho alichosema: " ukweli ni mambo fedheha, mdogo wetu chidi benzi cocaine au heroin / unga anaovuta unampeleka pabaya, tena mimi kama kaka yake namshauri aachane na matumizi ya madawa kulevya, kwa sababu mwisho wake utakua m'baya, mimi nilikua back stage na ikafika zamu yangu kupanda jukwaani nikawa naskia sauti mtu anatamba jukwaani kwa dakika saba ama nane, alikua ananichelewesha kupanda, na ananiharibia show yangu, huyu mtu si adui, nikatoa amri mara tatu kama F.F.U aka kaidi ndipo nikamfata na kumpa dozi, akaanguka chini na mimi nikaendelea na show yangu, hakuna hata mtu mmoja atakaye kubali kuharibiwa kazi, hata rais Kikwete ukimharibia utaishia jela."
Pia Msanii NASH MC a.k.a Kaka Suma nae pia aliweza kutoa maoni yake kuhusiana na sakata hilo kwa kuwaeleza watu kile kilichotokea ili watu waweze kufahamu yupi hasa alikuwa kinyume na mwenzie hadi kusababisha ugomvi huo; Nash aliandika maneno haya katika ukurasa wake wa facebook.

"nyimbo zako zimepigwa sana radioni,umefanya matamsha mengi sana nchini na nje ya nchi,umesifiwa sana katika vyombo vya habari,umepata mashabiki wengi,umetembea na kila aina ya mwanamke hapa mjini kwa umaarufu wako,kifupi ni kwamba umefanya mambo mengi sana katika kpindi cha umaarufu wako na hakuna aliekuja kukuingilia,siku nyingi sana nimekua nikilia na swala la nidhamu kwa wasanii wa kitanzania,upumbavu aliotuonesha chidi benz jana katika onesho la kalapina mpaka ikaelekea kupigwa kwake na nilikua nashuhudia yote aliyofanya ya kuvamia jambo ambalo halimuhusu tena kwa maneno ya dharau kabisa,akasema hajui kinachoendelea na hajui ni show ya nani..kwa kweli maneno hayo yalimchoma kila aliekuja pale na hakuna alieweza kumvumilia na baya zaidi aligoma kushuka hata kalapina alipomwambia kwa ustaarabu!! kipigo alichokipata alistahili na ni haki yake!!! nidhamu nidhamu nidhamu!!'

Alimaliza hivo Kaka Suma kwa kueleza ukweli huo.



Hapa chid Benz ndo alishaanza kuharibu mambo jukwaani kitu kilichopelekea mtata Kalapina kumfuata na kumpa kichapo
 

KALA PINA NA NASH MC WAELEZA NINI CHANZO CHA KUPIGWA KWA CHID BENZ Reviewed by Unknown on Tuesday, May 07, 2013 Rating: 5

No comments:

All Rights Reserved by Dj Mchomo © 2014 - 2015
Powered By WordPress24x7

Contact Form

Name

Email *

Message *

Dj Mchomo. Powered by Blogger.