Linex, Suma Lee & Baba Levo wapata ajali!
Taarifa iliyotufikia toka kwa msanii Linex ni kwamba akiwa na wasanii
wenzake Baba Levo na Suma Lee wamepata ajali wakielekea mkoani Kigoma
kikazi.
Kwa mujibu wa Linex, wakiwa wanaelekea kigoma ambapo watakuwa na show
wikiendi hii..walikutana na ajali hiyo lakini kwasababu hawakuwa na
mwendo kasi waliweza kusalimika.
Dancer mmoja wa Suma lee ameumia Mguu na Gari la Suma Lee ndio
lililoumia sana upande wa mbele,kwani taa zimepasuka na sehemu ya mbele
kuharibika sana.
Ajali ilisababishwa na basi la abiria lililokuwa katikati ya barabara
kwenye kona kali, ambapo ili kulikwepa lazima Suma angetakiwa atoke nje
ya barabara, ndipo gari ilipomshinda na kugonga mti.
Linex ,Baba levo na Suma lee wana show tatu weekend hii Ijumaa mjini Kigoma ,
Jumamosi ni Kasulu na Jumapili ni Bujumbura.
Linex, Suma Lee & Baba Levo wapata ajali!
Reviewed by Unknown
on
Wednesday, August 29, 2012
Rating:
No comments: