Sijafukuzwa bali Nimejiondoa - Suma
Siku chache baada ya mkurugenzi wa kampuni ya MTANASHATI, maarufu kwa
jina la Ostaz Juma na Musoma kutangaza kuwatimua ndani ya kampuni yake
msanii Suma Mnazaleti na aliyekuwa meneja wa wasanii aliyefahamika kwa
jina la Maneno, kisa akikitaja kuwa ni utovu wa nidhamu, Suma Mnazaleti
ameibuka na kusema kuwa hakufukuzwa bali yeye ameamua kujiondoa
mwenyewe.
Akinukuliwa kwa mdomo wake Suma Mnazareti, alisema..."Nimeamua
kujitoa mtanashati, na sababu kubwa katika zote ya kujitoa ni kwamba
nilifwata kazi kwa Ostaz na sio hela zake, so nilichokuwa nadhania
ntakipata mtanashati hakipo,Boss anatafta zaidi sifa na ustaa Tanzania
na mimi mziki ni kazi yangu.
Ostaz anaweza akagawa mamilioni kwa watu ili atajwe lakini anashindwa
kulipa hela ya maana kwa ajili ya video, matokeo yake anatoa shilingi
laki tatu? unadhani tutaweza kushindana na video kama za kina Ay za
million 30?. nimeuza mpaka balackberry yangu kuongeza kwenye pesa za
kukamilisha video yangu, wakati hata nilivyokua nahustle mwenyewe
sikuwahi kuuza simu yangu.
so nimejiondoa maana sioni faida yoyote, na mimi mziki kwangu ni masha nataka nifike mbele zaidi.
Kampuni ya Mtanashati inawamanage wasanii wazuri wengi tu kati yao ni kama Dogo janja, Amazon na PNC.
Sijafukuzwa bali Nimejiondoa - Suma
Reviewed by Unknown
on
Tuesday, August 28, 2012
Rating:
No comments: