Top Ad unit 728 × 90

Quick Rocka kufungua studio na record label yake

Rapper wa kundi la Rockers, Abbott Charles aka Quick Rocker amesema anaanzisha record label yake aliyoipa jina la 255.

Rapper huyo anayetamba na ‘club banger’ yake mpya iitwayo ‘Katika’ alisema pia anafungua studio yake ya kurekodi muziki aliyoipa jina la ‘Big Step’.

Akiongea na kipindi cha Block 4 Teen cha Down Town TV (DTV) weekend iliyopita, Quick alidai kuwa studio yake itapatikana maeneo ya Sinza jijini Dar es Salaam.

Hata hivyo hitmaker huyo wa ‘Bullet’ alisema pamoja na kuwa na studio yake mwenyewe, bado ataendelea kufanya kazi na studio zingine na kila aina ya producer ilimradi apate kitu kizuri.

Akiongelea wimbo wake mpya, ‘Katika’, Quick Rocker alieleza kuwa aliamua kutoka tofauti kwakuwa muziki wa Tanzania umebadilika ambapo watu wengi hupenda nyimbo zinazochezeka.

Katika mahojiano hayo, rapper huyo alizungumzia pia uwepo wa kundi lake la Rockers ambalo lilikuwa limevunjika na kudai kuwa kundi hilo limerudi tena na mashabiki wategemee mambo mapya.
Quick Rocka kufungua studio na record label yake Reviewed by Unknown on Thursday, September 13, 2012 Rating: 5

No comments:

All Rights Reserved by Dj Mchomo © 2014 - 2015
Powered By WordPress24x7

Contact Form

Name

Email *

Message *

Dj Mchomo. Powered by Blogger.