Top Ad unit 728 × 90

Kwa nini Muziki wa Dodoma haufiki Malengo?

Maoni ya wadau mbalimbali wa muziki wa Dodoma wameweza kuweka wazi kwamba muziki wa Dodoma unashindwa kufikia malengo kutokana na wasanii wenyewe kuwa hawako makini na kile wanachokifanya mwisho wa yote wananishia kulaumu media na vyanzo mbali mbali vya kuutangaza muziki wao.

Maoni hayo yameweza kutolewa na wasikilizaji waliokuwa wakitoa maoni yao katika kipindi cha Fleva Good Xtra ya Impact fm pale walipoulizwa ni nini hasa kinaufanya muziki wa Dodoma usifikie hatua ya ushindani na mikoa mingine ambao wanaonekana muziki wao unafika malengo.

Na pia idadi kubwa ya wasikilizaji walielekeza maoni yao kwa waandaaji wa muziki huo yaani ma producer ambao nao inasemekana bado hawajielewi ni nini wanatakiwa kuwafanyia wasanii wao ili waweze kufika hatua walizopo wenzao mpaka wanaitwa mastaa.

Pia wakati maoni hayo yakiendelea alifika msanii wa Dodoma anaetazamiwa kufanya vizuri katika muziki wa Ku-Rap hapa Tanzania anaekwenda kwa jina la Slim Sal na hapa chini ni maoni yake.
Kwa nini Muziki wa Dodoma haufiki Malengo? Reviewed by Unknown on Saturday, February 23, 2013 Rating: 5

No comments:

All Rights Reserved by Dj Mchomo © 2014 - 2015
Powered By WordPress24x7

Contact Form

Name

Email *

Message *

Dj Mchomo. Powered by Blogger.